Jumanne 19 Mei 2026 - 00:00
Vitisho dhidi ya Katibu Mkuu wa Nujabaa ni ishara ya kufilisika kwa Marekani/ Hongera kwa wapiganaji wa Iraq

Hawza/ Mwenyekiti wa Kamisheni ya Asili ya 90 ya Bunge la Ushauri la Kiislamu, huku akirejelea hatua ya Marekani kuweka zawadi ya dola milioni kumi kwa ajili ya taarifa kuhusu Sheikh Akram Al-Kaabi, alisema: Vitisho hivi vinatokana na hali ya kufilisika na kukwama kwa Marekani katika eneo hili, na tunawapongeza wapiganaji wa Iraq.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Hujjatul-Islam wal-Muslimin “Nasrullah Pezhmanfar”, Mwenyekiti wa Kamisheni ya Asili ya 90 ya Bunge la Ushauri la Kiislamu, huku akijibu hatua ya serikali ya Marekani kuweka zawadi ya dola milioni kumi kwa ajili ya kutoa taarifa yoyote kuhusu Sheikh “Akram Al-Kaabi”, Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Nujabaa, alisisitiza kwamba; hatua hii ya Washington ni ishara ya kina cha kufilisika na kukwama kwa Marekani katika eneo hili.

Akirejelea migogoro mikubwa ya ndani na ya kimataifa ya Marekani alisema: Marekani leo yenyewe, waziwazi na kwa siri, inakiri kwamba imefika katika mkwamo mgumu na iko ukingoni mwa kuporomoka kwa msukumo mdogo tu, si Marekani wala utawala wa Israel hawawezi tena kuendelea kwa njia ya kawaida, na matokeo yake tunaona katika eneo hili; kwa sababu hiyo, kutokana na hali ya kufilisika, wanatishia mkondo wa muqawama na Sheikh Akram Al-Kaabi.

Mwenyekiti wa Kamisheni ya Asili ya 90 ya Bunge alisisitiza: Bila shaka mhimili wa muqawama una makamanda na wanajeshi wengi ambao wote wanapigana kwa ushujaa, lakini ni muhimu kujibu suala hili na kutoa tahadhari muhimu kwa Marekani, kwa sentensi moja tunapaswa kusema: “Ewe nzi! Uwanja wa Simurgh si mahali pa kurukaruka kwako...!”

Hujjatul-Islam Pezhmanfar katika sehemu nyingine ya hotuba yake akiihutubia Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Nujabaa alisema: Hongereni! Mwenyezi Mungu akupeni nusura Inshaallah, hakika hapo kabla baadhi ya watu walikuwa na shaka kuhusu ulazima wa kusimama dhidi ya mkondo wa batili, leo mataifa yote duniani yamekubali kwamba njia pekee ni muqawama, Natumaini mtabaki daima imara, na sisi pia tuko pamoja na wapiganaji wa Iraq.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha