Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Kituo cha Utamaduni cha Iran kilichopo nchini Tanzania, kwa ushirikiano na jopo mashuhuri la wanazuoni wanaoheshimika kutoka nchi mbalimbali zikiwemo Tanzania, Kenya, Uganda, Nigeria, Afrika Kusini na Iran, kinakukaribisha kwa moyo mkunjufu kuhudhuria semina ya kitaaluma itakayo fanyika ana kwa ana mtandaoni tarehe 28 Aprili 2026 kuanzia saa 1:30 PM - 4:30 PM. Mjadala huo unalenga kuchunguza kwa kina fikra zenye ushawishi za Kiongozi Shahidi Seyyed Ali Khamenei (ra) kuhusu uhuru, heshima na mapambano ya muqawama, huku fikra hizo zikichambuliwa kwa mtazamo linganishi kati ya harakati za Iran na za Afrika, kama jukwaa linalojitolea kukuza ubadilishanaji wa kitamaduni na majadiliano ya kielimu, Kituo hiki kinaendelea kuimarisha ushirikiano wa maana kuhusu uzoefu wa pamoja wa kimataifa.
Semina hii imeandaliwa mahsusi kwa maprofesa, wahadhiri, watafiti, wanafunzi, na watu wote wenye shauku kubwa katika masuala ya kimataifa, uchambuzi wa kihistoria na fikra za kisiasa za kimataifa.
Semina hii ya mtandaoni inatoa fursa ya kipekee ya kushiriki katika majadiliano ya ngazi ya juu yanayolenga kuimarisha uelewa wa changamoto za pamoja za dunia na mitazamo ya siku zijazo.
Utaweza kujiunga katika kongamano hili kupitia kiunganishi kifuatacho:
https://meet.google.com/ntj-gcnp-rkw
Na kwa kufanya hivyo utakuwa sehemu ya mazungumzo yenye maana ya kielimu yanayounganisha mawazo na tajiriba kutoka mabara mbalimbali.
Maoni yako