Jumamosi 25 Aprili 2026 - 07:07
Tanzania yaandaa Shindano maalumu la kuchora kwa watoto kwa ajili ya kuwakumbuka watoto 168 waliouliwa kidhalim Iran

Hawza/ Kituo cha Utamaduni cha Iran, Jijini Dar es Salaam Tanzania, kimeandaa program maalumu ya shindano la uchoraji kwa watoto likiwa na lengo la kuwakumbuka wototo waliouliwa kidhamu na utawala wa Kizayuni pamoja na mshirika wake Marekani huko Minab nchini Iran.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, shule mbalimbali nchini Tanzania zimealikwa kushiriki katika shindano maalumu la uchoraji shindano ambalo litawahusu wanafunzi wa shule za msingi tu.

Lengo kuu na dhumuni la kuwekwa kwa shindano hilo ni kuenzi kumbukumbu ya wanafunzi 168 waliopoteza maisha yao huko Minab nchini Iran katika shule ya Shajarat Twayyibah, kufuatia shambuluo la kikatili lililofanywa na  utawala wa Marekani pamoja na mshirika wake Israel, shindano hilo linalenga kukuza matumaini, huruma na maadili ya kiroho kwa watoto ulimwenguni kote.

Shindano hili maalumu na la kipekee litawahusu wanafunzi wa darasa la kwanza hadi la sita, vile vile kituo hicho kimeagiza kwamba; kila mchoro uwe na jina la mwanafunzi, darasa lake na shule husika anayosoma.

Mwanafunzi anaweza kuwasilisha mchoro halisi au picha yake yenye ubora mzuri kupitia WhatsApp namba +255 625 560 570.

Washindi 30 watapata zawadi maalumu ambazo zimeandaliwa na Kituo cha Utamaduni cha Iran nchini Tanzania pamoja na vyeti.

Mwisho wa kuwasilisha picha hizo ni siku ya Jumanne, tarehe 27 Aprili 2026.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha