Alhamisi 9 Aprili 2026 - 16:20
Ammar Hakim apokea kusitishwa kwa mapigano na ametaka mazungumzo ya uhalisia kati ya Iran na Marekani

Hawza/ Hujjat al-Islam Sayyid Ammar Hakim, kiongozi wa Muungano wa Vikosi vya Kitaifa vya Iraq, amepongeza kusitishwa kwa mapigano katika vita dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

Kwa mujibu wa idara ya tarjama ya Shirika la Habari la Hawza, Ammar Hakim siku ya Jumatano alipokea kwa furaha kusitishwa kwa mapigano katika vita dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, na akasisitiza umuhimu wa kuheshimu mamlaka ya nchi na kutokikiuka uhuru huo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ofisi yake ya habari, Sayyid Ammar al-Hakim alitoa wito wa kuwepo kwa umakini na uhalisia katika mazungumzo yajayo kati ya Iran na Marekani, na akaeleza matumaini yake kuwa; mazungumzo hayo yatafikia amani ya kudumu na yenye uthabiti katika eneo hili, yatazuia kujirudia kwa matukio kama hayo, na kuwalinda watu wa eneo hilo, wakiwemo wa Iraq, dhidi ya majanga ya vita na athari zake za uharibifu.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha