Jumapili 16 Novemba 2025 - 22:48
Sheikh Ahmad Al-Qattan: Adui Yetu Ni Mmoja Tu, na Huyo ni Israel

Hawza / Mwanazuoni wa Kisunni nchini Lebanon amesisitiza kuwa: “Tuna imani na kitu kimoja tu, nayo ni imani yetu kwa nchi yetu; na tunaye adui mmoja tu, mabae ni Israel.”

Kwa mujibu wa ripoti ya Kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, Sheikh Ahmad al-Qattan, mwenyekiti wa Jumuiya ya Qawluna wal-Amal na mwanazuoni wa Kisunni nchini Lebanon, katika msimamo wake wa kisiasa kutoka mji wa Bar Elias katika eneo la Bekaa, alisisitiza kuwa: “Imani yetu ni mojatu nayo ni kwa taifa letu; na adui wetu ni mmoja — adui wa Kizayuni ambaye hana chembe ya utu.”

Alionesha masikitiko yake juu ya uwepo wa baadhi ya watu miongoni mwa “wenzeke katika taifa” ambao wanaposoma, wanasoma tu kitabu cha adui; na wanapoona, wanaona tu kwa macho ya adui. Akasema kuwa watu hawa hawatambui ulazima wa kuwa imara na kubakia Lebanon — jambo ambalo ni lazima ili kuilinda nchi yetu mbele ya changamoto zote.

Sheikh al-Qattan alisema kwamba tajriba zetu na adui huyu zinaonesha wazi kwamba yeye ni adui wa ubinadamu; kile alichokifanya Palestina kinaonesha kwa uthabiti ukatili wake, na kwamba hana utu wala huruma.

Mwanazuoni huyo wa Kisunni wa Lebanon aliongeza kwa kusema: “Tunawaambia watu hawa kuwa sharti mrudi mkahakiki upya misimamo yenu; na msome ‘kitabu cha utukufu na heshima’ — kitabu kinachotufundisha kuwa katika kukabiliana na adui huyu lazima tuwe imara, tuwe na umoja wa kitaifa na Kiislamu, na tuilinde nguvu yetu na kuilinda jamii yetu iliyo moja.”

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha