Jumanne 26 Agosti 2025 - 19:58
Majlisi ya mwisho katika mwezi wa Safar yafanyika kwenye Markazi ya Fiqhi Aimmat At-hār huko London

Hawza / Hafla ya maombolezo ya kumbukumbu ya kufariki kwa Mtume wa Uislamu (saw) na pia kumbukumbu ya kuuwawa kishahidi Imam Hasan al-Mujtaba (as) na Imam Ridha (as) zimefanyika katika ofisi ya marehemu Ayatollah Fazel Lankarani mjini London, mji mkuu wa Uingereza

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kifo cha kusikitisha cha Mtume wa rehema na mleta ufanisi kwa wanadamu, Muhammad Mustafa (saw), na pia kumbukumbu ya kuuwawa kishahidi kwa wanawe watukufu — Imamu wa pili Hasan al-Mujtaba (as) na Imamu wa nane wa Shia duniani, Ali bin Musa al-Ridha (as) — majlisi ya maombolezo ilifanyika katika ofisi ya marehemu Ayatollah Fazel Lankarani na Markazi ya Fiqhi ya Aimmah At-ṭahār mjini London, kwa kuhudhuriwa na kundi la waombolezaji wenye mapenzi, waliojawa huzuni na wafuasi wa Ahlul-Bayt wa Isma (as).

Hujjat al-Islam wal-Muslimin Sayyid Husayn Husayni Qummi, mwalimu wa hawza na chuo kikuu, katika hafla hii alifafanua kuhusu sira ya Mtume na fadhila za Imamu wa pili Hasan al-Mujtaba (as) na Imamu wa nane wa Shia duniani, Ali bin Musa al-Ridha (as), na alisisitiza juu ya ulazima wa watu kuiga kutoka kwao.

Kusomwa kwa aya za Qur’ani Tukufu, kusomwa kwa Ziara ya Ashura, uimbaji wa marthiya na kutaja msiba wa Ahlul-Bayt wa Isma(as), pamoja na kuswaliwa kwa Swala ya Jamaa na kufanyika kwa maadhimisho ya wageni, vilikuwa miongoni mwa vipengele vya hafla hii tukufu yenye muonekano wa kimaanawi.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha