Ijumaa 11 Septemba 2026 - 22:15
Kuwafunga maulama kwa kesi za maonesho ni dhuluma ya wazi dhidi yao, dini na nchi

Hawzah/ Maulama wa dini na viongozi wa Mapinduzi ya Kitaifa ya Bahrain wamesisitiza kwamba: Maulama wenye heshima na waumini nchini Bahrain hawajafanya kosa lolote, isipokuwa kusema: “Mola wetu ni Mwenyezi Mungu,” na kuwakamata ni sawa na kuifunga dhamiri.

Kwa mujibu wa Idara ya tarjama ya Shirika la Habari la Hawza, maulama wa dini na viongozi wa Mapinduzi ya Kitaifa ya Bahrain wanaoshikiliwa katika Gereza Kuu la Jaw, katika taarifa ya pamoja wamesisitiza kwamba: Maulama wenye heshima na waumini nchini Bahrain hawajafanya kosa lolote, isipokuwa kusema: “Mola wetu ni Mwenyezi Mungu,” na kuwakamata ni sawa na kuifunga dhamiri.

Wamesema: Kuwafunga maulama wa dini kupitia mashauri ya maonesho, ni dhuluma kubwa na ya wazi dhidi yao, familia zao, dini yao na nchi yao nzima.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wametaka kusitishwa hatua hizi za kiholela na kuachiwa huru watu wote waliokamatwa na wafungwa.

Taarifa hiyo imetiwa saini na watu wafuatao: Sheikh Ali Salman, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Al-Wefaq ya Kitaifa ya Kiislamu; Abdulhadi al-Khawaja, mwanaharakati wa haki za binadamu; Abdulwahab Hussein, kiongozi wa kimapinduzi; Sheikh Abduljalil al-Miqdad; na Sheikh Muhammad Habib al-Miqdad.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha