Jumatatu 25 Mei 2026 - 14:30
Kuwahudumia wananchi na kutatua matatizo ni wajibu muhimu zaidi wa viongozi

Hawza/ Hadhrat Ayatullah Nouri-Hamadani amesisitiza kuwa; leo hii, kazi muhimu zaidi ya viongozi wa mfumo wa Kiislamu ni kuwahudumia wananchi na kufanya juhudi za kutatua matatizo yaliyopo.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Dkt. Ali Darabi, Naibu Waziri wa Turathi za Utamaduni, Utalii na Sanaa za Mikono nchini Iran, amekutana na kufanya mazungumzo na Hadhrat Ayatullah Nouri-Hamadani.

Katika mkutano huo, Hadhrat Ayatullah Nouri-Hamadani, huku akirejelea historia ya kazi ya Dkt. Darabi, alielezea kuhudumia wananchi kuwa ndiyo wajibu muhimu zaidi kwa viongozi katika mfumo wa Kiislamu na akasema: "Kwa utambuzi wa muda mrefu niliokuwa nao juu yako, nasema kuwa, Alhamdulillah, wewe ni miongoni mwa viongozi waliofanikiwa katika mfumo wa Kiislamu, na popote ulipokuwa, lengo lako limekuwa ni kuwahudumia wananchi, ambapo leo hii kazi muhimu zaidi ni huduma hii kwa wananchi na jitihada za kutatua matatizo yaliyopo."

Marjaa huyu wa taqlid pia amepongeza shughuli na kazi za uandishi za Dkt. Darabi.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha