Kwa mujibu wa ripoti ya kitengo cha kimataifa cha Shirika la Habari la Hawza, kipindi cha televisheni “Upeo wa Ushindi; Mwisho wa tawala ya Marekani na Kuibuka kwa mfumo Mpya wa Dunia” kilifanyika siku ya Jumatatu tarehe 4 May 2026 kwa juhudi za Majma’ ya Kimataifa ya Qadimun, kwa ushiriki wa kundi la shakhsia za kidini na kisiasa kutoka nchi mbalimbali, na kilirushwa kupitia vituo vya Al-Kawthar na Safir.
Sheikh Abdullah Jabri, Katibu Mkuu wa Harakat al-Ummah nchini Lebanon, katika hotuba yake huku akirejelea hali ya eneo hilo alisema: Yale yanayoonekana leo katika uwanja wa mabadiliko ni makabiliano mapana kati ya mikondo mbalimbali, ambayo vipimo vyake vinazidi migogoro mdogo tu, na yana mizizi ya kina cha kihistoria na kifikra.
Akiweka mkazo juu ya umuhimu wa kuelewa kwa usahihi mabadiliko haya, aliongeza: Kutambua kwa usahihi hali halisi iliyopo na kuzingatia misingi ya kihistoria kunaweza kusaidia katika kuchambua vyema hali na kuchukua maamuzi sahihi.
Kiongozi huyu wa Lebanon aliendelea kusisitiza umuhimu wa kuimarisha mshikamano kati ya jamii za Kiislamu na akasema: Ummah wa Kiislamu licha ya kuwa na tofauti za mitazamo, una mambo mengi ya pamoja ambayo yanaweza kuwa msingi wa ushirikiano na muafaka.
Sheikh Jabri akirejelea uwezo uliopo katika ulimwengu wa Kiislamu alibainisha: Rasilimali za asili, uwezo wa kiuchumi na nafasi za kimkakati za nchi za Kiislamu zimeandaa fursa muhimu kwa ajili ya kuendeleza ushirikiano.
Aidha, alisisitiza umuhimu wa kusimamia tofauti na kuepuka mvutano wa ndani na akasema: Tofauti hazipaswi kuwa kizuizi cha ushirikiano, bali zinaweza kuelekezwa kupitia mazungumzo na mwingiliano katika njia ya maslahi ya pamoja.
Katibu Mkuu wa Harakat al-Ummah katika sehemu nyingine ya hotuba yake alielezea umuhimu wa kuwa macho mbele ya changamoto na akasema: Katika hali tata ya sasa, kuzingatia umoja, mazungumzo na kuimarisha kuaminiana ni mambo yenye umuhimu wa kipekee.
Mwishoni, akielezea matumaini yake kuhusu mustakabali, alibainisha: Kwa kutumia vyema uwezo uliopo na kuimarisha muafaka, inawezekana kufuata njia ya maendeleo na utulivu katika eneo hili.
Maoni yako