Jumanne 14 Aprili 2026 - 08:25
Vita ya tatu ya kulazimishwa, ni utetezi wa Mapinduzi na watu wa Iran pamoja na wapiganaji wa Uislamu/ Kipaumbele cha leo ni harakati za wanahawza

Hawza/ Mkurugenzi wa hawza nchini Iran, akirejelea shughuli za ziada na zenye thamani za madrasa za kidini na vituo vya usimamizi vya mikoa katika Vita ya Ramadhani, alisisitiza: Shughuli za kawaida za hawza za kielimu ziendelee kufuatiliwa, lakini suala la vita ya tatu ya kulazimishwa na utetezi wa kishujaa wa watu wa Iran na wapiganaji wa Uislamu liwe katika kipaumbele.

Kwa mujibu wa ripoti ya mwandishi wa Shirika la Habari la Hawza kutoka Tehran, Ayatollah A‘rafi, mkurugenzi wa hawza za kielimu za nchi, tarehe 24 Farvardin (13 April 2026), katika mkutano na mkurugenzi, manaibu na wakurugenzi wa kituo cha usimamizi wa hawza ya mkoa wa Tehran, na katika kikao cha kamandi ya vita mseto “ufikishaji ulio wazi” ya hawza za kielimu, huku akirejelea kuuawa kishahidi kiongozi wa Umma, Ayatullah Al-udhma Imam Khamenei, alisema: Kuuawa kishahidi kwa kiongozi mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu kumesababisha kuimarika kwa roho ya kujitolea na kujitoa muhanga miongoni mwa taifa kubwa la Iran.

Watu wa Tehran, kwa uongozi na usimamizi wa wanahawza, wameonesha ubora mkubwa katika Vita ya Ramadhani

Mjumbe wa Jumuiya ya Walimu wa Hawza ya Qum aliendelea kusema huku akirejelea uwepo wake katika mikusanyiko ya usiku ya wananchi: Tehran ni nguzo ya hema la Mapinduzi ya Kiislamu na nchi, na kwa hakika watu wa Tehran, kwa uongozi na usimamizi wa wanahawza, walionesha ubora mkubwa katika Vita ya Ramadhani. Walimu na wanafunzi wa madrasa za kidini pamoja na maimamu wa jamaa wa misikiti, wahubiri na makhatibu pia walitekeleza jukumu muhimu katika mikusanyiko ya usiku na katika kutetea Mapinduzi ya Kiislamu na nchi.

Mkurugenzi wa hawza za kielimu nchini Iran, aliendelea kwa kusema kuwa; hawza za kielimu zinapaswa kuimarisha roho ya ustahimilivu na kujitolea miongoni mwa wanazuoni wa dini, akasema: Leo, kipaumbele cha shughuli za wanahawza ni suala la vita ya tatu ya kulazimishwa na utetezi wa Mapinduzi ya Kiislamu na nchi.

Shughuli za kawaida za hawza ziendelee kufuatiliwa

Mjumbe wa Baraza Kuu la hawza za kielimu, huku akirejelea shughuli za ziada na zenye thamani za madrasa za kidini na vituo vya usimamizi vya mikoa katika Vita ya Ramadhani, alisisitiza: Shughuli za kawaida za hawza za kielimu ziendelee kufuatiliwa, lakini suala la vita ya tatu ya kulazimishwa na utetezi wa kishujaa wa watu wa Iran na wapiganaji wa Uislamu liwe katika kipaumbele.

Sote tunapaswa kumtii Walii al-Faqih

Katika sehemu nyingine ya hotuba yake, alirejelea utendaji mzuri wa baadhi ya madrasa za kidini, mabalozi wa uongofu na vituo maalumu vya mkoa wa Tehran katika nyanja za kielimu na utafiti, na akasema: Bila shaka jukumu la kituo cha usimamizi wa hawza ya mkoa wa Tehran katika kupata mafanikio haya linastahili kuthaminiwa.

Mkurugenzi wa hawza za kielimu mwishoni aligusia suala la kuimarisha nafasi ya uongozi katika hali ya sasa ya nchi na akakumbusha: Mafanikio ya kujivunia ya taifa la Iran katika Vita ya Ramadhani yametokana na mipango na mtazamo wa mbali wa kiongozi shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, na hivyo basi, sote tunapaswa kumtii Walii al-Faqih.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha