Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Katika muendelezo wa mfululizo wa kutoa ahadi kwa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu kutoka kwa wanazuoni, wanafunzi, na taasisi mbalimbali za kidini na zisizo za kidini, waalimu hawa wa hawza kutoka Qum, Khorasan, Isfahan, na mikoa mingine nchini Iran wameonesha mshikamano wao na Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Hatua hii ya wanazuoni inaonesha uhusiano wa kina na wa kudumu kati ya wanafunzi wa hawza na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Ahadi hii ya walimu hawa wengi kutoka Qum, Khorasan, Isfahan, na mikoa mingine inaonesha msaada wa wanazuoni kwa njia ya Mapinduzi ya Kiislamu na uongozi wa Kidini wa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi.
Harakati hii inahusiana na kuendeleza njia ya wanazuoni wakubwa wa Kiislamu katika kuunga mkono mfumo wa Kiislamu na kuonesha upya mshikamano na malengo ya Imam Khomeini (rah) na Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi.
Mwisho wa Taarifa
Maoni yako