Kwa mujibu wa ripoti ya kitengo cha tafsiri cha Shirika la Habari la Hawza, Ellison, mtoto wa Larry Ellison, mmoja wa waanzilishi wa Oracle na mfadhili mkubwa zaidi wa kifedha kwa utawala wa Kizayuni wenye kiu ya damu, baada ya kumbadilisha mkurugenzi wa kituo cha CBC, wale wasanii na waigizaji ambao walionesha kusimama na wananchi wanyonge wa Ghaza na kuyalaani mauaji ya kikatili ya Israel, amewaweka katika orodha nyeusi ya Hollywood na amedai kuwa Israel itawachukulia hatua za kisasi.
Watu hawa waovu wamechukulia hatua yao hii kama moja ya njia za kisasi za Israel dhidi ya barua iliyosainiwa na wasanii mwezi Septemba ya kutaka kususiwa vyombo vya habari vya Kizayuni kutokana na mauaji ya kimbari yanayoendelea Ghaza.
Kwa hakika, orodha hii nyeusi nchini Marekani inaendelea kuongezeka, na kila siku wasanii zaidi wanaunganishwa humo. Marekani ni mahali ambapo kuunga mkono haki za Wapalestina kunazidi kuchanganywa na hotuba za chuki, kwani wanafunzi wa vyuo vikuu wamepoteza ufadhili wao wa masomo kwa sababu ya kusimama na wananchi wanyonge wa Palestina; wanachama wa bodi za ufundishaji wamesimamishwa au kufukuzwa; na mashirika yote ya wanafunzi yamefukuzwa au kutangazwa kuwa yasiyo halali kwa sababu ya kupinga ziara za maafisa wa Israel.
Chanzo: Middle East MONITOR
Maoni yako