Jumatano 30 Julai 2025 - 15:57
Marekani na Israel Wameususia Mkutano wa Umoja wa Mataifa kwa Ajili ya Kuiunga Mkono Palestina

Hawza/ Mawaziri wa nchi kadhaa walikusanyika katika Umoja wa Mataifa ili kutafuta suluhisho la pande mbili kwa ajili ya kumaliza vita vya Ghaza na Israel, lakini Marekani na Israel walisusia mkutano huo.

Kwa mujibu wa ripoti ya Idara ya tarjuma ya  Shirika la Habari la Hawza, Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwaka uliopita, ukiwa na wanachama 93, uliamua kuandaa mkutano huu, na Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, alisema: “Lazima tuwe makini ili mkutano huu, tofauti na iliyopita, usigeuke kuwa maonyesho ya matangazo na maonyesho yasiyo na matokeo, bali uwe ni hatua ya kweli ya kusonga mbele.”

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa pia alihudhuria mkutano huu na akasema: “Vita vya Ghaza na Israel vimeuweka usalama wa dunia katika hali ya matatizo, tunapaswa kupata suluhisho la kina kwa ajili ya kusitisha vita hivi.”

Mohammad Mustafa Nakht, Waziri wa Palestina katika Ukingo wa Magharibi, pia aliyaomba mataifa yote kushughulikia haraka hali ya dharura ya Ghaza na kusisitiza: “Watu wote duniani, popote walipo, wanapaswa kuheshimiwa, na haki ya mamlaka ya kila nchi na watu lazima iheshimiwe. Watu wa Palestina hawawezi kuendelea kuwekwa kando tena.”

Chanzo: Reuters

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha