Ijumaa 20 Februari 2026 - 08:00
Rais wa Maldives atangaza mwongozo wa kimaadili katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

Hawza/ Rais wa Maldives, Dkt. Mohamed Muizzu, katika hotuba yake kutokana na mnasaba wa kuingia Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, ameutangaza mwezi huu kuwa ni fursa adhimu ya kuleta mabadiliko chanya nchini. Amesema kuwa; Ramadhani ya mwaka 1447 Hijria inapaswa kuwa mwezi wa mwongozo wa ujenzi na maendeleo kwa taifa.

Kwa mujibu wa Kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, Mohamed Muizzu, Rais wa Maldives, aliwapongeza wananchi wa Maldives pamoja na Umma wa Kiislamu kwa kuwadia Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Alisisitiza umuhimu wa kuzingatia faradhi, adabu, hukumu, sheria na kanuni za mwezi huu nchini Maldives, na akasema kuwa kuijenga jamii inayoswali mara tano kwa siku, inayowalea vyema watoto na vijana wake, na inayowaheshimu wakubwa wake, ndio msingi wa maadili na utawala bora kwa taifa.

Aidha, aliielezea jamii bora kuwa ni ile isiyo tumia dawa za kulevya na mazoea mabaya, inayofuata misingi ya Kiislamu na maadili ya kitamaduni.

Dkt. Mohamed Muizzu aliongeza kuwa; serikali inaunga mkono aina yoyote ya shughuli zinazoendeleza maadili na tunu za Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Pia alisisitiza kuwa mikusanyiko ya kijamii na kifamilia kama vile futari na daku huchangia kuimarisha mahusiano ya kijamii, huruma na mapenzi ndani ya mwezi wa Ramadhani.

Chanzo: PSM News

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha