Jumamosi 14 Februari 2026 - 22:00
Tugeuze Kongamano la Kitabu Bora cha Hawza kuwa chombo cha kimkakati cha kuongoza tafiti za Hawza

Hawza/ Mkurugenzi wa Hawza za nchini Iran, alisisitiza nafasi ya kimkakati ya Hawza katika kujenga ustaarabu mpya wa Kiislamu, huku akisema: tunapaswa kufanya Kongamano la Kitabu Bora cha Hawza liwe chombo cha kimkakati cha kuongoza tafiti za Hawza.

Kwa mujibu wa mwandishi wa SShirika la Habari la Hawza, Ayatollah Alireza Arafi, leo kabla ya adhuhuri, katika Kongamano la Ishirini na Saba la Kitabu Bora cha Hawza na Tamasha la Tisa la Makala za Kielimu za Hawza lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Madrasa ya Shule ya Kiislamu ya Imam Musa Kazim, huku akiuenzi mwezi wa Shaaban, kuzaliwa kwa Hujjatullah al-A‘zam (a.t.f.s.), na siku za Mungu za muongo wa mapinduzi (Fajr), aliwashukuru wanazuoni, walimu, watafiti na wasomi wa Hawza kwa kushiriki katika kongamano hilo.

Pia alitoa shukrani kutokana na ujumbe na maelezo ya Ayatollah al-udhma  Javadi Amoli, akawapongeza washindi wa sehemu za kitabu, makala na tasnifu, na kuwashukuru wachapishaji, taasisi za kielimu zilizopata nafasi za juu, pamoja na waandaaji, majaji na watendaji wa sekretarieti ya kongamano la Kitabu Bora cha Hawza.

Kuchora ustaarabu mpya wa Kiislamu; dhamira ya kimkakati ya Hawza

Mkurugenzi wa Hawza za kielimu, huku akirejelea tamko la “Hawza inayoongoza na bora”, alieleza kwamba mhimili wa tano wa waraka huo ni “ubunifu wa kiustaarabu katika mfumo wa ujumbe wa kimataifa wa Uislamu.” Alisema kuwa; katika waraka huo muhimu, Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ameutaja mhimili huu kuwa matarajio makubwa zaidi kutoka Hawza.

Akirejelea hotuba za kihistoria za mwanzilishi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ruhollah Khomeini, baada ya shambulio la utawala wa Pahlavi dhidi ya Madrasa ya Fayziyyah mwaka 1963, alisisitiza kwamba; wakati huo kuzungumzia kuanzishwa kwa ustaarabu wa Kiislamu kulionekana kwa baadhi kuwa ndoto kubwa; lakini muda ulionyesha kuwa imani na subira huondoa vikwazo, na sunna ya Mwenyezi Mungu hushinda njama za maadui.

Aliongeza kuwa: kuanzishwa kwa ustaarabu mpya wa Kiislamu ndio lengo kuu la kidunia la Mapinduzi ya Kiislamu, na Hawza ina jukumu zito katika njia hii; kwanza ichore muundo wa ustaarabu huo, kisha ifafanue, iusambaze na kuujenga kitamaduni. Huu ni mfano wazi wa “ufikishaji ulio wazi”.

Ayatollah Arafi alibainisha kuwa; falsafa ya Kiislamu inapaswa kupanua athari zake katika masuala ya kijamii ya Umma, na fiqhi pia inapaswa kupanua upeo wake kwa ubunifu katika istinbat ya masuala mapya ili kubainisha hukumu na mifumo ya kiustaarabu.

Muhammad Baqir al-Sadr; mbunifu wa fikra za Kiislamu za kisasa

Mkurugenzi wa Hawza alifafanua nafasi ya kielimu na kimapinduzi ya Ayatollah Sayyid Muhammad Baqir Sadr na kumtambulisha kama mmoja wa wabunifu wakubwa wa fikra za Kiislamu katika zama za kisasa. Akiashiria kuwa aliuawa kishahidi akiwa na umri wa miaka 47 au 48, alisema: kipaji na ukubwa wake wa kielimu ni wa kiwango kwamba leo maoni yake mapya yana nafasi muhimu katika masomo ya fiqhi, usul, kalam na tafsiri.

Akirejelea kazi zake maarufu kama Falsafatuna na Iqtisaduna, alisema: vitabu hivi, katika kipindi ambacho fikra za kiliberali na kijamaa zilikuwa zimetawala mazingira ya kielimu ya ulimwengu wa Kiislamu, vilibadilisha mizani ya fikra na kuipa harakati ya Kiislamu nguvu mpya ya kielimu.

Alisisitiza kuwa; Shahid Sadr alizifahamu kwa kina fikra pinzani, alizieleza kwa uadilifu na usahihi, kisha akazijibu kwa uchambuzi wa kina na wa kimfumo. Hakuwa tu katika nafasi ya kujihami, bali aliwasilisha nadharia mbadala za Kiislamu na kuchukua msimamo wa kimkakati na wa kushambulia katika mijadala ya fikra.

Alitaja sifa zake bora kuwa ni pamoja na kufahamu mijadala ya vyuo vikuu na kimataifa, uwezo mkubwa wa ijtihad, kalamu na hotuba yenye athari, na kuwasilisha mbinu mpya katika falsafa, uchumi, mantiki ya istikra na tafsiri ya Qur’ani. Aliongeza kuwa; angeweza kujitenga na mkondo wa Mapinduzi ya Kiislamu, lakini alitoa maisha yake yote kwa kumuunga mkono Imam na mapinduzi.

Ayatollah Arafi alisema: katika karne moja iliyopita, tukiwahesabu watu mashuhuri wa fikra za Kiislamu, baada ya Imam Khomeini na Allameh Tabatabaei, Shahid Sadr hung’aa kama jua lenye mwanga.

Kumuenzi Ayatollah Mohammad Ali Fayyazi na nafasi ya Kitabu Bora cha Hawza

Katika hafla hiyo pia alienziwa Ayatollah Fayyazi. Ayatollah Arafi, akirejelea zaidi ya nusu karne ya juhudi za kielimu za mwanazuoni huyo, alimtaja kuwa miongoni mwa nyuso zenye athari katika Hawza.

Kuhusu Tamasha la Kitabu Bora cha Hawza alisema: Kitabu Bora cha Hawza ni kioo cha tafiti za Hawza, ingawa bado hakionyeshi uwezo wote wa kielimu uliopo. Ni lazima tutoke katika hali ya kujihami katika kuwasilisha mafanikio ya kielimu na kugeuza tukio hili kuwa chombo cha kimkakati cha kuongoza mustakabali wa tafiti za Hawza.

Aliongeza kuwa; tamasha hilo linapaswa kuwa rejea ya kitaifa na kimataifa katika fikra za dini na kuwa na athari katika uongozi wa elimu na uzalishaji wa fikra.

Mabadiliko mapya katika Hawza za kielimu

Ayatollah Arafi alitaja baadhi ya hatua mpya katika Hawza, zikiwemo:

1. Kuendeleza fiqhi ya kisasa
2. Kuanzisha kamati za uongozi wa elimu katika fiqhi ya mifumo na fikra za hikma
3. Kuanzisha masomo ya juu ya utafiti katika nyanja sita za kielimu
4. Kuimarisha hatua ya pili ya darsi kharij
5. Kutoa uhalali rasmi kwa matini na masomo ya jadi yaliyo na mizizi
6. Kuchapisha mkusanyiko wa juzuu nyingi kuhusu historia ya miaka mia moja ya Hawza
7. Kupanua taaluma na masomo ya darsi kharij katika majimbo
8. Kubuni mfumo wa watafiti, upangaji wa viwango na uelekezaji wa tafiti
9. Kuzingatia kwa makini maendeleo ya akili bandia na uhusiano wake na elimu za Kiislamu

Mwisho, Mkurugenzi wa Hawza alisisitiza nafasi ya walimu na wanafunzi vijana katika kujenga mustakabali wa Hawza, kwa kusema: ukubwa wa mabadiliko ya kielimu na maswali mapya katika ngazi ya kitaifa na kimataifa ni mkubwa sana, na unahitaji juhudi maradufu za kizazi kipya cha Hawza ili tuwe na uwepo hai na wenye athari katika medani za fikra na ustaarabu.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha