Jumanne 23 Septemba 2025 - 06:38
Mmelifurahisha Taifa na Kuiinua Heshima ya Nchi

Hawzah/ Mtukufu Ayatullah Khamenei, katika ujumbe wake wa pongezi kwa Timu ya Taifa ya Mieleka ya Farangi kutokana na ushindi wao wa ubingwa wa dunia, aliwashukuru wanamichezo, makocha na viongozi kwa kulifurahisha taifa na kuiinua heshima ya nchi.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, matini ya ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ni kama ifuatavyo:

Bismillahir Rahmânir Rahîm

Nawapongeza vijana mashujaa wa mieleka ya farangi.

Azma thabiti na juhudi ngumu zenu pamoja na ndugu zenu wa mieleka ya Azad, zimei furahisha jamii na kuipa nchi heshima, namuomba Mwenyezi Mungu awajalie utukufu na ushindi, na ninatoa pongezi kwa mwanamichezo, kocha na meneja.

Sayyid Ali Khamenei
30 Shahrivar 1404 Hsh

Timu ya Taifa ya Mieleka ya Farangi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, baada ya miaka 11 na kwa mara ya pili, imeweza kusimama kwa uimara katika jukwaa la ubingwa wa dunia katika mashindano ya Zagreb 2025.

Hii ni mara ya kwanza katika historia ya michezo ya Iran ambapo Timu ya Taifa ya Mieleka ya Azad na ya Farangi zimefanikiwa kwa pamoja kutwaa ubingwa wa dunia katika mashindano ya kipindi kimoja.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha