Jumapili 8 Juni 2025 - 21:30
Chuo Kikuu cha Michigan Chaajiri Wapelelezi kwa ajili ya kuwasumbua wanafunzi wanaoiunga Mkono Palestina

Hawza/ Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Michigan nchini Marekani wameripoti kuhusu kuajiriwa kwa watu wanaowafuatilia mchana na usiku, kurekodi mazungumzo yao na kuwapa vitisho.

Kwa mujibu wa ripoti ya kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Michigan nchini Marekani waliokuwa wakishiriki kwenye maandamano ya kuiunga mkono Palestina na watu wa Ghaza, wamesema kupitia mahojiano mbalimbali kwamba chuo hicho kimewaajiri watu ili kuwafuatilia, kuwachukua video na picha, kurekodi mazungumzo yao ya kila siku, na kuwapeleleza. Upelelezi huo unafanyika si tu ndani ya chuo, bali hata nje ya chuo pia unaendelea.

Kwa mujibu wa gazeti la "The Guardian" la Uingereza, wanafunzi waliokuwa wakipinga hatua hiyo pia wameeleza kuwa upelelezi na udhibiti huo umefikia kiwango cha kuwa mbinu ya unyanyasaji na vitisho.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha