Ijumaa 6 Juni 2025 - 07:41
Kampeni ya Kimataifa ya “Khomeini ni kwa ajili ya watu wote” yafanyika; Ujumbe wa Imam waenea katika Upeo wa Mataifa

Hawzah/ Katika maadhimisho ya mwaka wa kumbukumbu ya kufariki kwa Imam Khomeini (ra), kampeni ya kimataifa ya “Khomeini kwa Wote” ikiwa na hashtag (#KhomeiniForAll) imeakisi ujumbe wake wa kimataifa kwa ushiriki mpana wa watumiaji kutoka kote duniani.

Kwa mujibu wa taarifa ya kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, sambamba na mwaka wa kumbukumbu ya kufariki kwa mwasisi mkubwa wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Imam Ruhullah al-Mūsawī al-Khomeinī (ra), kampeni ya kimataifa ya “Khomeini kwa Wote” imezinduliwa kwa mara ya nane mfululizo na taasisi ya “Harakati ya Husseini.” Kampeni hii ilianza tarehe 2 Juni na itaendelea hadi tarehe 8 Juni, ambapo maelfu ya watu kutoka pembe mbalimbali za dunia wanamuenzi Imam Khomeini (ra) kwa kushiriki kwa njia hai katika mitandao ya kijamii.

Katika mkondo wa kampeni hii, tagi ya #KhomeiniForAll (Khomeini kwa Wote) imekuwa miongoni mwa mitindo maarufu katika nchi mbalimbali kama India, Iran, nchi za Ulaya, Nigeria, na maeneo tofauti ya bara la Asia na Afrika. Watumiaji wa mitandao ya kijamii wanashiriki kwa wingi katika maadhimisho haya kwa kusambaza maneno ya kudumu ya Imam Khomeini (ra), video za kihistoria, dhana za msingi za fikra ya muqāwamah, pamoja na athari zake pana juu ya harakati za ukombozi duniani kote.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha