Jumapili 6 Aprili 2025 - 17:56
Je! ni dhikri ipi iliyo na athari zaidi kuliko dhikri nyingine zote?

Hadhrat Ayatollah Jawadi Amoli aliweka wazi kwa kusema: Mnaweza kuwa mmewahi kusikia mara kwa mara kwamba kuna baadhi ya watu wanatafuta dhikri huku wakijiuliza: " Je! Ni dhikri ipi tuisome ili itukaribishe kwa Mwenyezi Mungu?" Baadhi miongoni mwa watu wazito na wenye maarifa waliwahi kuandika risala fupi na kusema: “Hakuna dhikri yenye athari kubwa baada ya kumdhukuru Mwenyezi Mungu, kama dhikri ya kifo na kukumbuka mauti.”

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Ayatollah Jawadi Amoli katika mazungumzo yake alizungumzia mada ya “Umuhimu wa kukumbuka mauti na nafasi yake katika kuleta uchamungu (taqwa)” na akasema:

“Mara kwa mara mmekuwa mkisikia kwamba baadhi ya watu wanatafuta dhikri, huku wakiuliza: 'Ni dhikri ipi itakayo tukurubisha na Mwenyezi Mungu?' na mfano wa hayo.

Baadhi ya wanazuoni wakubwa na wenye maarifa waliandika risala fupi, wakisema: Tumetembea sehemu nyingi, tumekutana na wanazuoni wengi, tumesoma na kusikia maneno mengi, lakini hatukuona dhikri yoyote yenye athari zaidi baada ya kumkumbuka Mwenyezi Mungu mtukufu kama vile kukumbuka mauti.

Hakuna dhikri yeyote ile baada ya kumdhukuru Mwenyezi Mungu inayo lingana na kukumbuka Mauti. Je! Unatafuta kitu gani hasa! Inatosha kwa mtu kukumbuka mauti, mauti ndiyo yanavunja matamanio ya kidunia, tukitaka kumkaribia Mwenyezi Mungu, ni lazima tukumbuke mauti.

"Tukitaka kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu, ni lazima tukumbuke mauti. Mwanazuoni huyu katika risala yake anasema: Sijaona dhikri yoyote yenye athari kubwa zaidi baada ya dhikri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kama kudhukuru mauti. Dhikri hiyo humfanya mtu kuwa mchamungu; kwani ikiwa mtu atakumbuka kifo, basi bila shaka hiyo si kazi rahisi kuondoka duniani mikono mitupu huku uso wake ukiwa umejawa na aibu, hilo ni jambo gumu sana, hivyo basi, kwa hali ya kawaida mtu huyo mda wote atakuwa anafikiria kuhusu uchamungu."

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha