Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, katika hafla ya uzinduzi wa bango la Kiarabu la harakati ya Qur’ani "Maisha kwa Aya", Sheikh Naim Qassem, akihutubia wasomaji wa Qur’ani, wahafidhi na watu wa Qur’ani Tukufu wa Lebanon, huku akisisitiza juu ya umuhimu wa kusoma, kutafakari na kuhifadhi Qur’ani Tukufu, alielezea matumizi ya mafundisho ya Qur’ani kuwa ni miongoni mwa njia muhimu zaidi za kutambua na kushiriki kikamilifu katika uwanja wa vita mseto vinavyoikabili leo dunia ya Uislamu dhidi ya ubeberu.
Hujjatul-Islam Muhammad Haj Abu al-Qassim pia, katika mkutano huu, alipofafanua harakati ya kitaifa ya "Maisha kwa Aya" nchini Iran, alisema: Harakati ya "Maisha kwa Aya" iliundwa kwa dhamira ya kuhakikisha kwamba mafundisho ya Qur’ani yanakuwa sehemu ya misingi ya fikra za watu, na kwamba nafasi ya dhana na mantiki ya Qur’ani Tukufu katika mfumo wa mahesabu na uelewa wa jamii iwe kubwa na yenye athari zaidi.
Mwanazuoni huyu wa Hawza na chuo kikuu aliendelea kusema: Tangu mwanzo wa kuanzishwa kwa harakati hii, makundi ya wananchi yamejitahidi kupitia uzalishaji wa maudhui ya Qur’ani, kielimu, kisanaa na kufuatilia lengo hili, na takribani Wairani milioni 13 walishiriki kikamilifu katika harakati hii katika mwezi mtukufu wa Ramadhani wa mwaka uliopita, jambo linaloonesha uhusiano wa kina wa wananchi wa Iran na mafundisho ya Qur’ani Tukufu.
Hujjatul-Islam Haj Abu al-Qassim alihitimisha kwa kusema: Kuanzishwa kwa harakati ya "Maisha kwa Aya" nchini Lebanon, iliyoundwa kwa juhudi za ndugu zetu wapendwa wa Hizbullah, kunahesabiwa kuwa ni hatua ya kwanza ya harakati hii ya Qur’ani katika uwanja wa kimataifa, na tunatarajia baraka za mafundisho haya ya Qur’ani ziwe nuru ya kuwaongoza Waumini wote katika njia ya mapambano, uimara na upinzani dhidi ya ubeberu.
Mwisho wa kikao hiki, bango la Kiarabu la harakati ya "Maisha kwa Aya" lilizinduliwa rasmi, na operesheni hii ya kitamaduni na Qur’ani ilianza rasmi katika nchi ya Lebanon.
Katika mkutano huu, mbali na Sheikh Naim Qassem, Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon, na Hujjatul-Islam Muhammad Haj Abu al-Qassim Doulabi, pia walihudhuria watu mashuhuri kama Sayyid Ali Fahs na Sheikh Talal miongoni mwa maafisa wa kitamaduni na Qur’ani wa Hizbullah ya Lebanon, pamoja na wengineo.
Maoni yako