Ijumaa 31 Oktoba 2025 - 10:12
Mwinyi Arejea Ikulu Kwa Kishindo, Masoud Apatwa na Butwaa + Picha

Mgombea wa Nafasi ya Rais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi  amechaguliwa tena kuwa Rais wa Zanzibar kufuatia Ushindi alioupata  katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 29 Oktoba 2025 dhidi ya mpinzani wake mkuu ndugu Othman Masoud Othman.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ( ZEC) Jaji George Joseph Kazi ametangaza Matokeo hayo  Tarehe 30 Oktoba 2025  kwenye Ukumbi wa Jaji Mkuu Mstaafu  Abdi Mahmoud, Afisi ya Tume ya Uchaguzi, Kilimani, Mkoa wa Mjini Magharibi. 

Akitangaza Matokeo hayo Jaji George Kazi amesema  Mgombea huyo wa Chama cha Mapinduzi ameshinda kwa kupata kura. 448,832 sawa na asimilia 74.8 ya Kura zote halali.

Shangwe, Nderemo, Vifijo  na Nyimbo za Hamasa  kutoka kwa Viongozi na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi  vikisikika ndani ya  ukumbi  baada ya Kuyapokea  matokeo hayo ya Ushindi yanayomrejesha tena Madarakani  Dkt. Hussein Ali Mwinyi kuiongoza Zanzibar kwa Awamu ya Pili.

Dkt. Hussein Ali Mwnyi aliyewania Kiti hicho kwa  Awamu ya Pili  amewashinda Wagombea wengine 10 wa Vyama Vya Upinzani  waliojitokeza  kugombea nafasi hiyo katika Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Jaji George Kazi alimkabidhi Dkt. Mwinyi  Cheti Maalum Cha Ushindi  wa  Urais wa Uchaguzi Mkuu.

Akizungumza baada ya Ushindi huo Rais Mteule Dkt. Hussein Ali Mwinyi  ameipongeza Tume ya  Uchaguzi kwa kazi nzuri ya kusimamia Uchaguzi huo pamoja na kuwapongeza Wagombea wa kiti cha Rais kwa kuonesha Uzalendo na kuwaomba kuweka mbele Uzalendo na Maslahi ya Taifa. 

Dkt. Mwinyi amewapongeza Wananchi wa Zanzibar kwa kuamua kwa mujibu wa katiba  kwa  kujitokeza kwa wingi kupiga kura. 

Aidha, amewashukuru  Wananchi kwa kufanya Uchaguzi kwa amani na utulivu wakatii wote wa Kampeni na siku ya Uchaguzi na Kuahidi kufanya kazi na wote walio tayari kushirikiana naye kwa Maslahi ya Nchi.

Mwinyi Arejea Ikulu Kwa Kishindo, Masoud Apatwa na Butwaa + Picha

Mwinyi Arejea Ikulu Kwa Kishindo, Masoud Apatwa na Butwaa + Picha

Mwinyi Arejea Ikulu Kwa Kishindo, Masoud Apatwa na Butwaa + Picha

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha