Jumamosi 12 Aprili 2025 - 17:46
Filamu ya mustanadi ya “Imamu Khamenei” imeandaliwa na channel ya Al-Manar ya Lebanon ni Riwaya ya Maisha ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu

Filamu ya mustanadi ya “Imamu Khamenei” iliyozalishwa na kituo cha Al-Manar nchini Lebanon, katika sehemu nane iliyoandikwa na Ayman Zughayb, inasimulia maisha ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, filamu hii, yenye jina “Khamenei”, ni kazi ya kituo cha Al-Manar Lebanon na inajumuisha sehemu nane, ambapo Ayman Zughayb ndiye mwandishi wake. Filamu hii inaangazia kipindi cha utotoni na ujana wa Imamu Khamenei, mahali alipoishi, alikokulia na kukomaa kifikra na kimalezi.

Pia, filamu hii inaeleza kuhusu nasaba na historia ya babu wa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya kiislamu katika maeneo mbalimbali kama vile Iraq, Iran, Hazaweh, Tafresh, Tabriz na Mashhad.

Filamu hii pia inaonesha historia ya elimu yake, masomo ya Hawza (vyuo vya kidini), pamoja na harakati zake dhidi ya utawala wa kidhalimu wa wakati huo, maisha yake ya gerezani na maeneo aliyopelekwa uhamishoni.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha