Jumapili 30 Machi 2025 - 11:07
Matembezi ya Siku ya kimataifa ya Quds nchini Niger  

Sambamba na Siku ya Kimataifa ya Quds, Waislamu waliokuwa wamefunga nchini Niger, katika Ijumaa ya mwisho ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, walishiriki kwenye matembezi hayo ili kuonyesha mshikamano wao na kuliunga mkono taifa la Palestina linalo dhulumiwa.

Kwa mujibu wa idara ya kimataifa ya  Shirika la Habari la Hawza, matembezi na hafla ya Siku ya kimataifa ya Quds yalifanyika katika mji mkuu wa Niger Niamey, kama ilivyokuwa katika mataifa mengine ya kiislamu, hafla hiyo ilihudhuriwa na balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, wanazuoni wa kishia, wahubiri, wanafunzi, na waislamu waliokuwa wamefunga katika chuo kikuu cha Al-Mustafa.  

Watu hao huku wakiwa kwenye mfungo walipaza sauti zao wakisisitiza mshikamano na umoja wao na Palestina dhidi ya wavamizi wa kizayuni na waungaji mkono wao madhalimu, huku wakidai ukombozi wa Quds Tukufu na ardhi ya Palestina.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha