Ijumaa 5 Desemba 2025 - 13:42
Mwenendo wa Malezi wa Ayatullah Kashmiri

Hawza/ Ayatullah Qaemi, mmoja wa wanafunzi wa Ayatullah Kashmiri, anaeleza utaratibu wake wa malezi kwa mtazamo wa Ayatullah Kashmiri, kufikia ukamilifu wa kiroho kunategemea hatua kuu mbili: ya kwanza ni kuacha kikamilifu mambo yote ya haramu, na ya pili ni kutekeleza kwa usahihi wajibu wa kidini.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Ayatullah Kashmiri, aliyekuwa arifu mashuhuri, alianza njia ya kuwalea wanafunzi wake kupitia hatua mbili za msingi: kuacha kabisa maharamisho na kutekeleza kwa makini wajibu wa kisheria.

Ayatullah Qaemi, mwanafunzi wake, anasema: “Kwa kawaida, ukamilifu unaowajia waja wa Mwenyezi Mungu hujitokeza baada ya hatua ya kuacha maharamisho na kufanya wajibu wa dini.”

Iwapo angeona kwamba mtu tayari amepita hatua hiyo, si mtu wa kufanya madhambi, na wala haachi hata wajibu mmoja, basi alikuwa akisema mambo mengine zaidi; mfano, anamuhusia mtu amuelekee Mungu zaidi, au angempa adhkari fulani, hapo ndipo alikuwa akianza.

Chanzo: Kitabu Sheydā, uk. 88

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha