Jumapili 2 Novemba 2025 - 23:23
Toleo la arobaini na nane la jarida “Dini na Uhusiano wa Kimataifa” limechapishwa; Kuanzia mwamko wa kiroho wa kidijitali hadi kurejea Rifā‘ī nchini Iraq

Hawza/ Toleo la arobaini na nane la jarida la kila mwezi “Dini na Uhusiano wa Kimataifa” limechapishwa kwa juhudi za Idara ya Mahusiano ya Kimataifa ya Vyuo vya Kidini kwa ushirikiano na Kituo cha Utafiti cha Mersād. Toleo hili limejikita katika kuchunguza mabadiliko ya kidini, kitamaduni na kijamii duniani, likichambua masuala mapya kuanzia zama za kidijitali hadi mageuzi ya Mashariki ya Kati.

Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Habari la Hawza, toleo jipya la jarida “Dini na Uhusiano wa Kimataifa” katika chapisho lake la arobaini na nane, limeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Idara ya Kimataifa ya hawza na Kituo cha Utafiti cha Mersād.
Toleo hili limeangazia mwenendo mpya wa kidini, kisiasa na kitamaduni katika uwanja wa kimataifa, likilenga kuchambua matukio ya ulimwengu wa sasa kwa mtazamo wa elimu ya kalam, ustaarabu, na diplomasia ya kidini.

Katika toleo hili, mada mbalimbali zimechapishwa, zikiwemo:

“Mwisho wa enzi ya Erbash; Arpagoosh na kujenga upya imani kwa Shirika la Dini.”

“Mipango ya kupinga Ushia nchini Malaysia; haja ya kuchunguza masuala ya nyakati za mwisho.”

“Mapadre wa akili bandia na mwamko wa kiroho wa kidijitali.”

“Kutoka katika wahy hadi skrini ya kifaa cha kidijitali; wajukuu wa Mtume wa Mwenyezi Mungu na dini ya kidijitali.”

“Askofu Mkuu wa kwanza mwanamke; kisa cha kipekee miongoni mwa viongozi wa dini duniani.”

“Utaifa wa Kihindu nchini Marekani; mambo sita ambayo kila mtu anapaswa kuyajua.”

Pia, mada nyingine zimejadiliwa kama vile:

“Kwa nini Jordan ilifunga Kituo cha Imamu al-Albānī?”

“Magharibi na fikra mpya kuhusu ndoa ya wake wengi,”

“Ushiriki wa mamia ya marabi wa Ulaya katika mkutano wa kihistoria wa Azerbaijan.”


Miongoni mwa makala nyingine katika toleo hili ni pamoja na:

Ripoti ya uchambuzi: “Ukristo chini ya ushawishi wa harakati ya MAGA.”

“Ufunguzi mpya wa Shule ya Orthodox ya Heybeliada; changamoto na matumaini baada ya ziara ya Ikulu ya White House.”

Jarida “Dini na Uhusiano wa Kimataifa” huchapishwa kwa lengo la kufuatilia na kuchambua mabadiliko ya kidini na kifikra duniani kwa mtazamo wa vyuo vya kidini, na linatambulika kama moja ya majarida ya kitaalamu katika utafiti wa dini na mahusiano ya kimataifa.

Kwa ajili ya kupata nakala ya kidijitali ya toleo hili na kusoma makala kamili, wapenzi wa jarida wanaweza kutembelea tovuti rasmi ya Idara ya Mahusiano ya Kimataifa ya Vyuo vya Kidini:

🆔 @howzehinternational

Maoni yako

You are replying to: .
captcha